Quantcast
Channel: Envaya: Latest updates
Viewing all articles
Browse latest Browse all 4212

BAKWATA WILAYA YA GAIRO added a News update.

$
0
0

ISLAMIC FUNDATION WAKABIDHI MSIKITI BAKWATA

Mwenyekiti wa tasisi ya The Islamic Foundation amekabidhi msikiti wa vibandani Morogoro Mjini. Makabidhiano hayo yalifanyika baada ya kukamilika kwa ujenzi huo na kufanyika ufunguzi rasmi wa msikiti huo uliopewa jina la Masjid Madina. akiongea mara baada ya ufunguzi huo Mwenyekiti wa Islamic Fondation aliwahusia Waislam kutumia vizuri msikiti huo ili iwe sababu ya wao kuingia peponi badala ya kuanza kugombania uongozi mpaka kufikia kuvunja mipaka ya Allah S.W
Akionggea Sheikh wa Mkoa wa Morogoro ambae pia ni Sheikh wa Wilaya ya Gairo alisema. waislam tuache kubaguana kwa kuwa sisi sote tupo katika njia moja ya Laila ha Ilallah hivyo tunapaswa kuungana kwa pamoja na kufanya yetu kama Waislam Chuki za Kitaasisi magovi baina ya Mtu na Mtu hayana maana badala yake tutumie misikiti yetu kama vituo vya kuendesha mambo yetu ya kidini. Tuache majungu. Mwisho Sheikh alitoa Shukran kwa Islamic Foundation kwa usimamizi mzuri wa ujenzi wa msikiti wa Kisasa.


Viewing all articles
Browse latest Browse all 4212

Trending Articles