Quantcast
Channel: Envaya: Latest updates
Viewing all articles
Browse latest Browse all 4212

ZANZIBAR SCOUTS ASSOCIATION (ZANSA) updated its History page.

$
0
0

Chama cha Skauti Ulimwenguni kilianzishwa na Mwengereza aitwae Sir Lord Baden Powel (BP) tangu mwaka 1907 huko uingereza katika kisiwa cha Brown sea, uskauti uliingia Zanzibar mwaka 1912 miaka 5 tu baada ya kuanzishwa na Sir lord Baden Powel.

Chama cha Skauti Zanzibar kimeanzishwa mwaka 1912 tangu ukoloni, baada ya Mapinduzi ya Zanzibar 1964 Mheshimiwa Rais wa kwanza hayati Abeid Amani Karume akaisitisha kuendelea kufanya kazi na kuona kwamba ni sehemu ya ukoloni kwa uskauti huo umeletwa na waingereza.

 

Hata hivyo mwaka 1992 Mheshimiwa Rais wa awamu ya tano Dr Salmin Amour Bin Juma alipokwenda Magila Mkoani Tanga katika jamboree na kuwaona vijana wa skauti, Mheshimiwa Rais alikuwa na shauku ikiambatana na furaha baada ya kuwaona vijana wa skauti katika mkoa huo papo hapo akaamua uskauti huo uwepo na visiwani Zanzibar ili vijana nao waweze kujifunza ubunifu, uzalendo na ukakamavu.

Kutokana na kauli hio ndio kwa mara ya pili uskauti ukafufuliwa na kuundwa kamati maalum ya kufufua Uskauti Zanzibar, chini ya wizara ya vijana katika serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa wakati huo.

 

Chama cha Skauti Zanzibar ni chama hiari, na wala hakifungamani na vyama vya siasa nchini lakini wala hakina chembe ya ubaguzi wa rangi dini wala jinsia.

 

Chama Cha Skauti Zanzibar huchangia elimu na Malezi kwa vijana kwa kupitia njia ya ‘Uskauti’ ambapo humjenga kijana kimwili, kiakili, kimtazamo, kijamii, kiimani iliaweze kujitegemea na kuwajibika na kumfanya kijana hujifunza mengi kwa vitendo kama Kusaidia jamii katika Majanga, kutoa huduma za jamii katika siku kuu za kitaifa, Uokozi, na kusaidia jamii katika ujenzi wa Taifa letu.

 

Chama Cha Skauti Zanzibar kitasimaimia harakati za wanachama wake katika ngazi zote za Mkoa, Wilaya na shehia ili kuhakikisha Vijana wa kiskauti kila siku wanatenda mema kwa jamii na kuhakikisha wanapata elimu ya kutosha kulingana na kanuni na Ahadi za Shirika la harakati za skauti Ulimwenguni (Wold organization Scouts Movement)

Iyeleweke kwamba suala la skauti ni suala la kitaifa na linajulikana Dunia nzima tangu ilipoasisiwa na mwanzilishi wake Sir. Lord Baden Powell.

imetoewa na

Rahma Mohammed Shariff

Kamishna Habari na Mawasiliano

Chama Cha Skauti Zanzibar

 


Viewing all articles
Browse latest Browse all 4212

Trending Articles