Asasi kwa kushirikiana na wanaasasi wae imeandaa mafunzo ya sheria ya malezi ya mtoto
kwa wanajamii wa kata ya Mpeta. Mafunzo hayo yamelengwa kuwasaidia wanajamii kuweza kufahamu umuhimu wa malezi kwaa mtoto na sheria zinazohusu masuala hayo. Mafunzo hayo
yatafanyika kati tarehe 10-14 za mwezi wa Septemba mwaka huu wa 2105 kwenye zahanati ya Mpeta. Wawezeshaji watakuwa ni Yakobo Mchopa, Mwanaafa Malenga, Anjelina Saidia na Thecla Mbawala.
Ni matumaini yetu kuwa wananchi wa kata hiyo na vijiji jirani wataweza kuhudhuria na kupata elimu hiyo itakayotolewa bure.