DAKEDEO KATIKA MAFUNZO YA UFURUTU ADA- MOROGORO.
DAKAWA ECONOMIC DEVELOPMENT ORGANIZATION Inashiriki katika mafunzo endelevu ya Mradi wa Kuzuia Ufurutu Ada (Violent Exitremism) ambayo yanaendeshwa kwa pamoja na shirika la GREEN LIGHT PROJECT.
Katika mafunzo hayo ambayo yalianza mwezi June 2017 mjini Tanga na yanayotarajiwa kukamilika Tarehe 27/03/2018 DAKEDEO imewakilishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa asasi Mr Msenga Amir A.
Lengo kuu la mafunzo haya ambayo yanawakilisha washiriki 40 toka katika mikoa ya Arusha Tanga, na Zanzibar ya na lengo la kuzijengea Uwezo CsO pamoja na Serikali juu ya mbinu za kukabiliana na UFURUTU ADA.
Katika mafunzo haya washiriki wametoka pia katika Taasisi za Kidini Madhehebu ya dini pamoja na washiriki toka katika Serikali kuu ngazi ya Mikoa.
Mafunzo haya yamegawanyika katika sehemu kuu tatu (Topics) 1. Matumizi ya dini katika kuchochea Ufurutu Kiada (Violent extremism) 2. Jamii ya makundi yaliotengwa katika katika UFURUTU ADA. 3. USHAWISHI KWA VIJANA.
Ni mategemeo ya DAKEDEO Kuwa Hapo mbeleni Asasi za kiraia zitashiriki vema katika miradi ya kuhakikisha kuwa Tanzania inaendelea kuwa nchi ya amani kwa kuendesha mafunzo endelevu kwa jamii.
Imetolewa na Mkurugenzi mkuu mtendaji.