Quantcast
Channel: Envaya: Latest updates
Viewing all articles
Browse latest Browse all 4212

Chanika Tuamke Youth Organization (CTYO) updated its History page.

$
0
0

 

CHANIKA TUAMKE YOUTH ORGANIZATION (CTYO)

S . L .P ……………. Simu na.+255718586804/+255713849524/+255621153354

Chanika Wilaya ya Ilala Dar es Salaam

Utangulizi

Chanika Tuamke Youth Organization (CTYO) Ni shirika lisilo la kiserikali lililoanzishwa rami tarehe 13/03/2005 likijulikana kama Tuamke Arts Group na kusajiliwa tarehe 15/01/2015 katika Wizara ya Maendeleo ya jamii jinsia na Watoto na kupata namba 00NGO/00006839 . Shirika linatekeleza shughuli zake katika Wilaya ya Ilala Mkoani Dar es salaam. Lengo kuu la CTYO ni kuwawezesha vijana kushiriki katika mipango,kusimamia na kuitekeleza ili kuleta maendeleo katika jamii.

CTYO Inafanya shughuli za Ushawishi na Utetezi     katika kuhakikisha utekelezaji wa haki ya Afya ya uzazi kwa vijanauzingatiwa wa maadili,malezi na huduma rafiki kwa vijana unazingatiwa.Shirika hili pia limelenga kufanya uchambuzi wa sera mbali mbali za vijana na kusimamia utekelezaji wake na Kutoa elimu ya Ujasiliamali kwa vijana.

Kanuni za maadili

  • CTYO ni Asasi isiyo ya kiserikali
  • Haifungamani na kabila lolote
  • Haitajihusisha na Siasa
  • Sio yenye kugawana faida

Muundo wa Uongozi

  • Mkutano Mkuu
  • Bodi ya wakurugenzi
  • Mkurugenzi
  • Katibu Mkuu
  • Mratibu wa Fedha na
  • Kamati ndogo ndogo

Usajili

CTYO imesajiliwa chiuni ya sheria ya NGO NA. 24 ya mwaka 2002 kama iivyofanyiwa marekebisho mwaka 2005.namba ya usajili 00NGO/00006839.

Eneo utendaji kazi

CTYO imesajiliwa kwa ngazi ya taifa na eneo la utendaji kazi Tanzania Bara ila kwa sasa tumeanza kufanya kazi katika kata mbilli za manispaa ya Ilala nazo ni; kata ya Chanika naZingiziwa .

Dira ya Asasi

Kuwa na vijana bora wanaoweza kupanga mipango, kuisimamia na kuitekeleza ili kujiletea maendeleo chanya.

Dhamira

Kufanya ushawishi na utetezi kuhakikisha kuwa vijana wanapata Afya,Maadili, Malezi na Huduma bora ya rafiki kwa vijana katika jamii na serikali kwa ujumla na kuchambua sera mbalimbali za vijana kuhakikisha kuwa sera hizo zinakwenda na wakati na kufanyiwa kazi.

Malengo ya CTYO

  • Kuwajenga uwezo vijana kujiajiri wenyewe
  • Vijana kujiakwamua kiuchumi
  • Kudhibiti maambukizi mapya ya virusi vya Ukimwi
  • Kukuza vipaji vya vijana katika michezo na sanaa
  • K uelimisha jamii juu ya afya ya Uzazi kwa vijana

Kuhakikisha kuwa vijana wanapata maslahi yao katika ngazi zote za serikali jamii kiujumla.

Walengwa

  • Vijana kuwanzia miaka 10-35
  • Vijana na watoto waishio katika mazingira hatarishi
  • Vijana n awatoto   waathirika na Virusi vya Ukimwi
  • Vijana wanaoishi katika mazingira magumu
  • Vijana wanaokinzana na sheria na vijana kwa ujumla.

Baadhi ya Mafanikio;

ü  Kuisajili Asasi kwa taratibu za sheria za NGO

ü  Kufungua Akaunti katika benki ya KCB

ü  Kufanya semina mbalimbali za Afya ya uzazi

ü  Tumefanikiwa kufanya mabonanza manne 4 ya Afya ya Uzazi kwa vijana

ü  Kujengewa uwezo na AMREF juu ya

ü  Kuandaa mpango kazi

ü  Kuandaa Bajeti

ü  Kuandaa taarifa ya utekelezaji na uwasilishaji

ü  Namna ya Uelimishaji wa jamii

ü  Namna ya Kuendesha Asasi.

ü  Kuviunganisha baadhi ya vikundi vya Bodaboda

Baadhi ya Changamoto:

ü  Rasilimali Fedha

ü  Uhaba wa vitendea kazi

ü  Upungufu wa waelimishaji Rika

ü  Ukosefu wa wafadhili wa kufadhili shughuli za CTYO

ü  Kuibiwa baadhi ya vitendea kazi

Mipango Endelevu

ü  Kuendelea kutoa Elimu ya Afya ya uzazi kwa vijana

ü  Kuendea kupambana na Makundi hatarishi kama

ü  Wafanya biashara ya ngono

ü  Vikundi vinavyo tumia dawa za kulevya

ü  Vikundi vya kamali na Bodaboda

ü  Kujengea uwezo vikundi mbalimbali vya kijamii katika suala zima la kujikwamua kiuchumi.

ü  Kuendelea kutoa elimu ya VVU na Ukimwi na kuamasisha jamii upimaji kwa hiari

ü  Kuendelea kupambana na Ukatili zidi ya watoto na wanawake

ü  Kufanya Ushawishi na Utetezi kuhakikisha kuwa kuna kuwa na Uwazi,Uwajikaji,na Utawala bora katika sekta ya Afya.

Njia zinazotumika kuwafikia walengwa

ü  Semina

ü  Midahalo

ü  Vipeperushi

ü  Sanan Shirikishi

ü  Kutembelea vituo vya serikali vinavyo toa huduma kwa jamii kama:

ü  Vituo vya Afya vya Serikali

ü  Vituo vya Elimu ya Serikali

ü  Ofisi za serikali za Mitaa,kata,wilaya,Mkoa na Taifa

ü  Kujengea Uwezo jamii kutambua haki za mteja katika kupata huduma ya Afya katika vituo vya   afya vya serikali.

ü  Kufanya Ushawishi na Utetezi kuhakikisha kuwa vijana wanapata masilahi yao katika jamii na serikali kwa ujumla.

ü  Kuwajengea uwezo vijana kujikwamua kiuchumi,kutoa elimu ya Ujasilia mali,kuwaunganisha vijana kuwa pamoja katika maamuzi na kuhakikisha kuwa tunaingiza agenda za vijana WDC

ü  Vyombo vya Habari

Mawasiliano/Mitandao ya kijamii kama

ü  Sms kampeini

ü  Facebook

ü  Twitter

ü  What’s App

ü  Instagram

Maombi kwa Wadau wa maendeleo ya vijana

Ndugu Mhe,Mdau wa maendeleo ya vijana tunatuma maombi yetu kwako juu ya mambo yafutayo:

Vitendea kazi vifuatavyo;

ü  Computer aina ya Laptop 2

ü  Printer 1

ü  Camera 1 na Rasilimali Fedha

ü  Projekta 1

Tunaimani kubwa uatatusaidia katika hili ili tukamilishe malengo.

Shukrani zetu kwako/kwenu

Ndugu mh, waheshimiwa tunatoa shukrani zetu za dhati kwako/kwenu kwa kutufutilia kwaribu sana ili kuhakikisha malengo yetu kama vijana yana kamilika.

Tunawashukuru sana wetu wafuatao kwa ukaribu wao kwetu

ü  Amref

ü  Mhe,Diwani mstaafu wa kata ya chanika

ü  Wenyeviti wa serikali za mitaa

ü  Aliye kuwa Mbunge jimbo la ukonga 2010

ü  Afisa maendeleo ya jamii wilaya ya Ilala. Afisa vijana wilaya ya Ilala.Ngao group na matumini group

Hitimisho

CTYO Ina kushukuru wewe kwa kutufuatilia kwa umakini sana.

Lakini pia CTYO ina vijana Makini,malidadi,

Waelevu,Wanaojiamini,Wanaoweza kupaga mipango,Kuisimamia na kuitekeleza ili kujiletea maendeleo na kuleta maendeleo katika jamii

 

 

 

 

 

 

 


 

 

 

Viewing all articles
Browse latest Browse all 4212

Trending Articles