Kuwa mjasiriamali wa Jamii (Be social entrepreneur).
Mara nyingi utakutana na vijana wengi wakitafuta kazi au wakisema wanataka kuanzisha biashara na miradi mbalimbali ila swali la muhimu la kujiuliza ni wito wa kufanya kazi au kuwa wafanyabiashara? Jibu lake halisi ni kuwa wamekosa kipto cha kujikimu, wamechoka kuwategemezi kwa familiaa zao, au kipato chao cha saasa hakiwatoshi, na maamuzi haya huwapata tu wanapo jiuliza swali hili "Nitapata pesa wapi za kunitosheleza?” na huamua kutafuka kazi za kuajiriwa, jitolea au kuanzisha biashara mbalimbali, Naamini kila mmoja anatamani kuishi maisha ya utoshelevu kwa kila kitu. “Ni mara ngapi unapohisi kwamba huna pesa za kutosha?”
Toka nilipopata maono ya kuanzisha Asasi ya PDPR na kufanikiwa kuendesha miradi kadha kiufanisi iliyonijengea jina ndani na njee ya nchi, Nikaanza kupokea barua zaidi ya 4 kwa siku za maombi ya kujitole (Volunteerism) kila muombaji niliyemuuliza kwanini ameamua kuchukua maamuzi hayo Majibu yake yalikuwa ni Hana kazi ya kufanya asubuhi hadi jioni, Anahitaji kipato au kipato cha ziada, anahitaji uzoefu na kuna wengine walikuwa na saababu zenye msingi kama za kuleta mabadiriko katika jamii yao kwa kutumia muda wao wa ziada au mapumziko. Sasa wewe toka uhitimu masomo yako umepata ajira, nafasi ya kujitolea au kuutumia ujizi wako kujiingizia kipato? Lahasha kama bado waweza ambatana nasi na utakuwa sehemu ya mabadiliko na watu wa mfano na kujivunia katika jamii yako.
PDPR ikaona ni vyema kuitumia rasirimali hii inayotafuta ajira, kipato na nafasi za kujitolea kuijengea uwezo na ikafanye miujiza kokote itakako kuwa si tu kuwapa nafasi ya kijitolea (Volunteer) bali kuwapa ujuzi, stadi na mbiu za kuiwezesha jamii kijikwamua na umasikini huku nao wakijiiingizia kiato. Ndipo ilipo anzisha WING OF CHANGES CAMPAIGN na SOCIAL ENTERPRENEUR INCUBATOR PROGRAM.
Wing of changes Campaign - hii ni kampeni inayofanywa na rafiki wa PDPR kwa ajiri yaa kusaidia miradi ya PDPR na jamii inayoizunguka, pia inasaidia upatikanaji wa fursa mbalimbali za kujitole, ajira, kulea, kuendeleza, kuwezesha, kufadhili na kuzamini hii inafanyawa sana na marafiki, wanaojitolea a washirrika waliopo njee za nchi.
Social Entrepreneur Incubator Program– ni mradi uliobuniwa kuwaendeleza vijana wa kitanzania wanaohitimu elimu ya sekondari na vyuo kuweza kuziona, kuvumbua, thubutu kuzitumia fursa mbalimbali zinazowazunguka hasa za kijamii, Matatizo na changamoto ni fursa kwa mtu mwenye ujuzi unaozitatua, PDPR inatoa elimu, mafunzo, ujuzi kwa walengwa na baada ya hapo inawaweka kambini na kuwapa stadi zingine za kuwawezesha kutimiza ndoto zao za kuisaidia jamii na wao kujikwamua kiuchumi na kisha kila wahusika wawili hadi watano wanapewa vitendea kazi na kuanza kutekeleza shughuli mbali mbali za kijamii wakisaidiwa na PDPR kwa mwaka mmoja kwa kupata mahitaji ya kimradi. Mradi huu sasa kila mwezi unasajiri zaidi ya watu 10 walio jitoa kuitumikia jamii. Je vifaa, gharama za kuendesha zinatoka wapi? Zinatoka katika mradi wa Wing of Changes Campaign. Walengwa wote walio tayari wanasaidiwa kuanzisha asasi zao, vyama vya kijamii, vyama vya ushirika vya kuweka na kukopa, vikundi vya kiuchumi, kupata mafunzo ya utengenezaji bidhaa za kijasiriamali kama batiki, vikoi, sabuni, mishumaa, ushonaji. PDPR kwa sasa inashirikiana na Msazi community Organization ya Malawi kupitia Mkurugenzi wake Hastings Phiri wa Mzimba kutafuta fursa mpya na masoko wa mradi huu. Wanufaikaji wanapewa cheti, kitambulisho, vitendea kazi na wanunganishwa na wa bia wa maendeleo wa PDPR.
Fursa zipi za kijamii zinapewa kipaumbele kwa sasa?
1) Mobile ICT training,
2) Kuwajengea uwezo wakulima juu ya kilimo cha kisasa, ujasiriamali, utunzaji wa kumbukumbu.
3) Kuwaelimisha vijana juu ya HIV/AIDS, kilimo, ufugaji kuku na fursa za kibiashaa na uwekezaji.
4) Nishati endelevu, (Renewable energy) tuna wabia wetu wanfundisha utengenezaji wa wind turbine, biogas, nk.
5) Kilimo cha matunda, mbogaamboga, usindika naa ufungashaji.
6) Utengenezaji wa mashine ndogo ndogo kupitia PDPR Development center.
7) Kusaidia uanzishwaji wa SACCOSS, VICOBA, makampuni NK.
8) kuwasaidia kuanzisha mradi wa uchimbaji wa visima vya maji na ufugaji wa kuku na samaki.
Wabia wa mradi huu ni kampuni ya MABOMA, Tanzania care, ARUPA, wafadhili wa mradi, na wanachama wa WING OF CHANGES CAMPAIGN.
“Anza leo kutaka kufanikiwa na kesho bado utajishangaa mwenyewe ukisha fanikiwa”
Karibu sana uwe sehemu ya mabadiliko.
Mfunzo na huduma zinatolewa bure.