Quantcast
Channel: Envaya: Latest updates
Viewing all articles
Browse latest Browse all 4212

ASASI YA UKOMBOZI WA VIJANA TANZANIA ( AUVITA) added a News update.

$
0
0

TUNAIENZIJE SIKU YA MAZINGIRA?Umepanda mti leo?

Leo ni siku ya mazingira duniani ambayo inatukumbusha kuwa uhai wetu inalindwa na mazingira yetu, hivyo tukiwa kama wadau katika sekta ya mazingira tunawakalibisha wadua na wahifadhi mazingira ili kuu tetea uhai wetu kwani kuishi kwetu kunategemea mazingira yetu.

Nikweli kabisa kuwa hatunabudi kuyalinda na kuyahifadhi mazingira yetu na kuienzi siku hii kwa fulaha kwani inatupa matumaini mapya ya kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabia ya nchi yanayo itikisa Dunia.

Mazingira yetu ni uhai wetu tuyalinde yatulinde. kama hatutaona umuhimu wa kuyalinda mazingira basi tunamtizamo wa kuyakatisha maisha yetu, Pamoja na uhifadhi wa mazingira tunayaweka mazingira ya uhai wa viumbe wengine katika hali safi yaani uhifadhi wetu wa mazingira unayaboresha si tu maisha ya binadamu bali na viumbe wengine.

Siku hii iwe chachu ya kutujengea misingi bora ya kuyaheshimu maeneo yaliyotengwa sehemu mbalimbali nchini kwa kuendelezwa kimazingira na kuyaheshimu maeneo haya, serikali hainabudi kushughulikia suala la mgawanyo wa maeneo yatuzungukayo kulingana na matumizi na kuzisimamia sheria kikamilifu.

Pia jamii ifahamu kuwa uhifadhi wa mazingira ni jukumu la kila mtu na inatupasa kushiriki wote kakamilifu juu ya suala zima la kuyahifadhi mazingira yetu.

Uhai wetu ni mazingira yetu tuyalinde yatulinde


Viewing all articles
Browse latest Browse all 4212

Trending Articles